About the Journal
Jarida la Dira ya Lugha (JADILU) lilianzishwa mwaka 2023. Hili ni jarida la kimataifa linalochapisha makala zake mara mbili kwa mwaka. JADILU ni jarida linalolenga kuchochea mijadala inayohusu Taaluma za Kiswahili zikiwemo isimu, lugha, fasihi pamoja na taaluma zinazohusiana nazo kama vile tafsiri na ukalimani. Jarida hili ni njia muhimu ya kusambaza maarifa yanayoibuliwa na tafiti mbalimbali za taaluma za Kiswahili. Jarida linapatikana katika nakala ngumu pamoja na nakala tepe ya mkondoni.
Lengo kuu la JADILU ni kukuza, kueneza na kutandawaza lugha ya Kiswahili na utamaduni wa Mswahili na Mwafrika. Hivyo, tunahimiza wanazuoni, watafiti na wataalamu mbalimbali kutuma makala za taaluma zote za Kiswahili, Tafsiri, Ukalimani na Utamaduni wa Kiswahili kutoka kote duniani kuchapishwa katika jarida la Dira ya Lugha. Tunapokea miswada iliyoandikwa kwa Kiswahili na Kiingereza na inayohusu taaluma za Kiswahili na Kiafrika.